Saturday, May 11, 2013


SUA PRIMARY PROGRAM


COMMUNICATION OFFICER ADRESSING
 CLIMATE CHANGE ISSUES
Siku ya tar. 8/5/2013 TFSA likwenda kufanya semina fupi,  ya mabadiliko ya tabia nchi (Climate change) katika shule ya msingi SUA.


Semina hiyo ilikuwa ni ya darasa moja, darasa la sita lakini pia kulikuwa na wanakikundi, kikundi cha mazingira cha shuleni hapo.


Watoa mada walikuwa ni Shaabani, Salim – TFSA GS na William Charles – TFSA COMMUNICATION OFFICER



TFSA-GS
asking questions to students


Wanafunzi hao walielimishwa yafuatayo:-

  • Nini maana ya tabia nchi,

  • Nini maana ya mabadiliko ya tabia nchi,

  • Mabadiliko ya tabia nchi yanasababishwa na nini?

  • Athari za madiliko ya tabia nchi na

  • Nini kifanyike ili kupunguza tatizo hilo la mabadiliko ya tabia nchi




Wanafunzi walishiriki semina vizuri kwa kuchangia katika baadhi ya waliyokuwa wanayafahamu na pia walishiriki kwa kujibu maswali na wanafunzi waliojibu maswali vizuri walizawadiwa daftari na peni. Wanafunzi hao ni Muhati, Asheri, Eriki, Magomola, Hamisi, Charles, Shangwe, Petronila, Ester na Agness.

wanafunzi wa shule ya msingi SUA

MSHIRIKI AKIPEWA ZAWADI






SUA TV RECORDING PROGRAM 2

Tarehe 10th May 2013 tuliendelea na program ya kurekodi vipindi mbalimbali vya kuelimisha jamii katika kituo cha televisheni, SUA-TV. Mara hii tulizungumzia mada ya kilimo mseto (Agroforestry)
Washiriki katika program hiyo walikuwa, Mauki, Dickson-3rd year., Msangi, Joyce-3rd year., Milkajane, Sangiwa-2nd  year na Samweli William Sikoi
Kipindi hicho kihusu mada ya kilimo mseto ambapo yafuatayo yalizungumziwa;

1.   Kilimo mseto ni nini?
·      Maana ya kilimo mseto?
·      Mifano ya maeneo katika Tanzania yanayofanya kilimo mseto
·      Kwanini maeneo hayo yanatumia njia hiyo ya matumizi ya ardhi?
2.   Kuna mifumo mingapi ya kilimo mseto?
·      Taja idadi ya mifumo iliyopo
·      Elezea kwa undani kila aina ya mfumo ulioutaja hapo juu
3.   Faida ya kutumia kilimo mseto kama matumizi sahihi ya ardhi.
4.   Changamoto zinazokabili kilimo mseto

Ushauri kwa jamii wenye uhaba wa ardhi na wasiokuwa na uhaba wa ardhi

No comments: